Ujerumani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Bundesrepublik Deutschland
Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani
Bendera ya Ujerumani Nembo ya Ujerumani
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Einigkeit und Recht und Freiheit
(Kijerumani: "Umoja na Haki na Uhuru”)
Wimbo wa taifa: Wimbo wa Wajerumani (beti ya tatu)
Umoja na Haki na Uhuru
Lokeshen ya Ujerumani
Mji mkuu Berlin
52°31′ N 13°24′ E
Mji mkubwa nchini Berlin
Lugha rasmi Kijerumani 1
Serikali
Rais
Chansella (Waziri Mkuu)
Shirikisho la Jamhuri
Joachim Gauck
Angela Merkel
Dola Takatifu la Kiroma

Dola la Ujerumani
Shirikisho la Jamhuri
Maungano
843 (Mkataba wa Verdun)

18 Januari 1871
23 Mei 1949
3 Oktoba 1990
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
357,050 km² (ya 63)
2.416
Idadi ya watu
 - 2014 kadirio
 - 2011 sensa
 - Msongamano wa watu
 
80,716,000 (ya 16)
80,219,695
226/km² (ya 58)
Fedha Euro (€) 2 (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .de
Kodi ya simu +49
1 Kideni, Kijerumani cha Kaskazini, Kisorbia, Kifrisia ni lugha rasmi katika mikoa kadhaa 2 hadi 1999: Mark (DM)



Ujerumani (pia: Udachi, kwa Kijerumani: Deutschland) ni nchi ya Ulaya ya Kati.

Imepakana na Denmark, Poland, Ucheki, Austria, Uswisi, Ufaransa, Luxemburg, Ubelgiji na Uholanzi.

Ni nchi yenye watu wengi katika Ulaya, isipokuwa Urusi ina watu zaidi.

Uchumi wa Ujerumani una uwezo mkubwa: ni nchi inayouza bidhaa nyingi nje kushinda mataifa yote ya dunia.

Muundo wake kiutawala ni shirikisho la jamhuri lenye majimbo 16 ndani yake na kila jimbo lina kiwango cha kujitawala.

Lugha asilia ni Kijerumani kinachojadiliwa kwa lahaja mbalimbali, lakini wenyeji wote wanasikilizana. Katika maeneo mawili kuna wasemaji asilia wa Kideni na Kisorbia.

Wahamiaji wa karne ya 20 wameleta lugha zao, hasa Kituruki na lugha za Ulaya ya Kusini.

Upande wa dini, Wakristo ni 66.8% (Wakatoliki 30.8%, Walutheri 30.3%, Waprotestanti wengine 5.7%), huku Waislamu wakiwa 1.9%. Thuluthi moja ya wakazi haina dini yoyote.

Jina la nchi

Wenyeji wanaiita "Deutschland" (De-Deutschland.ogg Deutschland (info), tamka: doich-land) na jina hilo limeingia katika Kiswahili kama "Udachi". Lilikuwa jina la kawaida katika karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20.

Siku hizi neno "Ujerumani" limechukua nafasi yake kutokana na Kiingereza kinachoiita "Germany".

Jiografia

Ujerumani unaenea kati ya bahari upande wa kaskazini na milima ya Alpi upande wa kusini.

Mipaka yake upande wa magharibi na mashariki ilibadilika mara nyingi katika historia yake; tangu mwaka 1945 mpaka wa mashariki ni mto Oder. Upande wa magharibi sehemu ya mpaka ni mto Rhein.

Kuna kanda tatu za kijiografia:

  • tambarare ya pwani ya kaskazini
  • kanda ya vilima
  • milima ya kusini pamoja na Alpi.

Tambarare ya pwani ya kaskazini ni eneo bapa; hakuna milima na nchi haipandi juu ya mita 200, sehemu kubwa ni kati ya uwiano wa bahari na mita 60 juu yake.

Historia

Miji

Majiji yenye wakazi zaidi ya milioni moja ni:

Miji mikubwa mingine ni:

Majimbo

  1. Flag of Baden-Württemberg.svg Baden-Württemberg
  2. Flag of Bavaria (lozengy).svg Bavaria (Freistaat Bayern)
  3. Flag of Berlin.svg Berlin
  4. Flag of Brandenburg.svg Brandenburg
  5. Flag of Bremen.svg Bremen (Freie Hansestadt Bremen)
  6. Flag of Hamburg.svg Hamburg (Freie und Hansestadt Hamburg)
  7. Flag of Hesse.svg Hesse (Hessen)
  8. Flag of Mecklenburg-Western Pomerania.svg Mecklenburg-Pomerini (Mecklenburg-Vorpommern)
  9. Flag of Lower Saxony.svg Saksonia Chini (Niedersachsen)
  10. Flag of North Rhine-Westphalia.svg Rhine Kaskazini-Westfalia (Nordrhein-Westfalen)
  11. Flag of Rhineland-Palatinate.svg Rhine-Palatino (Rheinland-Pfalz)
  12. Flag de-saarland 300px.png Jimbo la Saar (Saarland)
  13. Flag of Saxony.svg Saksonia (Freistaat Sachsen)
  14. Flag of Saxony-Anhalt.svg Saksonia-Anhalt (Sachsen-Anhalt)
  15. Flag of Schleswig-Holstein.svg Schleswig-Holstein
  16. Flag of Thuringia.svg Thuringia (Freistaat Thüringen)

Watu maarufu


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Denmark | Estonia | Hispania | Hungaria | Ireland | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituania | Luxemburg | Malta | Poland | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Ufalme wa Muungano | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Flag Germany template.svg Makala hii kuhusu maeneo ya Ujerumani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ujerumani kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.