Amerika ya Kaskazini
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Amerika ya Kaskazini ni bara kwenye upande wa Kaskazini mwa Ikweta. Inapakana na Bahari ya Pasifiki upande wa Magharibi, na Bahari ya Atlantiki upande wa Mashariki.
Ina nchi mbili hadi tatu kutegemeana na hesabu :
- Kanada
- Marekani
- Meksiko ni kijiolojia sehemu ya Amerika Kaskazini ingawa kiutamaduni ni sehemu ya "Amerika ya Kilatini" na kuhesabiwa pia katika Amerika ya Kati.
Kisiwa cha Greenland ni sehemu ya Amerika Kaskazini kijiografia maana kipo juu ya bamba la gandunia lileile lakini si nchi huru kipo chini ya Denmark.
Nchi za Amerika ya Kati zinahesabiwa kuwa sehemu za bara hilo katika hesabu ya kawaida ya bara saba. Kijiolojia ziko juu ya bamba la gandunia tofauti na Amerika Kaskazini ni bamba la Karibi pia kihistoria na kiutamaduni ziko toafuti na nchi mbili kubwa katika kaskazini.
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Amerika ya Kaskazini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |