Ukraine
|
|||||
Kaulimbiu ya taifa: -- | |||||
Wimbo wa taifa: Ще не вмерла України Shche ne vmerla Ukrajiny]] "Ukraine's glory has not perished" |
|||||
Mji mkuu | Kiev (Kyiv) |
||||
Mji mkubwa nchini | Kiev | ||||
Lugha rasmi | Kiukraine | ||||
Serikali | Demokrasia Petro Poroshenko Arseniy Yatseniuk |
||||
Uhuru ilitangazwa Kura ya maoni ya wananchi ilikubaliwa |
24 Agosti 1991 1 Desemba 1991 25 Desemba 1991 |
||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
603,700 km² (ya 44) 7% |
||||
Idadi ya watu - 2014 kadirio - 2001 sensa - Msongamano wa watu |
44,291,413 (ya 32) 48,457,102 73.8/km² (ya 115) |
||||
Fedha | Hryvnia ya Ukraine (UAH ) |
||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
EET (UTC+2) EEST (UTC+3) |
||||
Intaneti TLD | .ua | ||||
Kodi ya simu | +380
- |
Ukraine (Україна, Ukraina) ni nchi ya Ulaya ya Mashariki. Imepakana na Urusi, Belarus, Poland, Slovakia, Hungaria, Romania na Moldova.
Kuna pwani ya Bahari Nyeusi na ghuba ya Azov.
Lugha na utamaduni[hariri | hariri chanzo]
Kiukraine (українська мова "ukrajin's'ka mova") ni lugha rasmi, lakini angalau nusu ya wakazi hutumia Kirusi. Kiukraine ni lugha ya Kislavoni karibu sana na Kirusi.
Kwa muda mrefu Ukraine ilitawaliwa na Urusi na Kirusi kilikuwa lugha ya utawala hali halisi.
Tangu uhuru serikali imeendesha sera ya kujenga lugha ya kitaifa, pamoja na kujali lugha nyingine 18 za kieneo.
Wakazi[hariri | hariri chanzo]
Sensa ya mwaka 2001 ilionyesha ya kwamba 77.8% za wakazi hujiita "Waukraine". Waliojiita Warusi walikuwa 17.3%. Vikundi vingi vingine kama Wabelarus, Wamoldova, Watartari, Wabulgaria, Wapoland, Wayahudi na wengine walikuwa kila kimoja chini ya 1%.
Baada ya ukomunisti kupiga vita dini kwa njia zote na kwa miaka mingi, siku hizi wakazi wengi hawana dini yoyote.
Walionayo ni hasa Wakristo wa Kanisa la Kiorthodoksi la Russia, lakini Waorthodoksi wengine wamejitenga na kuanzisha Kanisa la Kiorthodoksi la Ukraina.
Pia kuwa waamini wengiwengi wa Kanisa Katoliki, hasa wa Kanisa Katoliki la Kigiriki la Ukraina linalofuata mapokeo ya Kigiriki kama Waorthodoksi, lakini pia wa Kanisa la Kilatini.
Pamoja na hayo, idadi ya wakazi inazidi kupungua haraka.
Historia[hariri | hariri chanzo]
Kwa muda mrefu Ukraine ilikuwa sehemu ya Dola la Urusi.
Miaka 1918 - 1921 baada ya mwisho wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia na ya kuporomoka kwa Dola la Urusi nchi ilikuwa na kipindi kifupi cha uhuru na vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Miaka 1922 - 1991 Ukraine ilikuwa jamhuri mwanachama wa Umoja wa Kisovyeti.
Hatimaye ilijipatia tena uhuru wake, ingawa Russia haijaridhika wala kukubali mipaka. Hivyo mwaka 2014 ilivamia rasi ya Krimea na maeneo mengine ya mashariki.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- (Kiingereza) Tovuti ya serikali
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Ukraine kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
|