Guyana ya Kifaransa
Région Guyane | |
---|---|
Jina la Kifaransa | Région Guyane |
Jina la kawaida | Guyana ya Kifaransa |
Mji Mkuu | Cayenne |
Eneo | 83,534 km² |
Mkuu wa Mkoa | Rodolphe Alexandre |
Idadi ya wakazi | 250,109 |
Sensa ya mwaka | 2013 |
Wakazi kwa km² | 3 |
Wilaya (arrondissements) | 2 |
Ramani Reunion na Ufaransa bara |
Guyana ya Kifaransa (kwa Kifaransa: Guyane française au Guyane pekee) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa ("département d'outre-mer" au DOM) katika Amerika Kusini.
Imepakana na Brazil na Surinam.
Pwani ya Bahari ya Karibi (Atlantiki) iko upande wa kaskazini.
Ilikuwa koloni la Ufaransa; sasa imekuwa sehemu kamili ya Ufaransa kisiasa na kisheria. Wakazi ni raia wa Ufaransa. Eneo lina hali ya mkoa (departement) na pia kanda (region) katika Ufaransa. Hivyo Guyane ni sehemu ya Umoja wa Ulaya. Pesa yake ni Euro.
Makao makuu ya Guyane ni mji wa Cayenne.
Watu[hariri | hariri chanzo]
Idadi ya wakazi imekadiriwa kuwa 250,109 katika mwaka 2013.
Wakazi walio wengi ni wa asili ya Afrika au wa mchanganyiko wa Kiafrika-Kizungu (60-70%). Asilimia 14 ni Wazungu; wengine ni Waindio asilia (3-4%), Wachina (3-4%), Wahindi na wahamiaji wa hivi karibuni kutoka Laos (1-2%).
Lugha rasmi na ya kawaida ni Kifaransa.
Upande wa dini, wakazi walio wengi ni Wakatoliki.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini |
Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyana ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela |
Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Guyana ya Kifaransa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |