Roma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Mji wa Roma
Collage Rome.jpg

Bendera

Nembo
Mji wa Roma is located in Italia
<div style="position: absolute; z-index: 2; top: Expression error: Unexpected < operator.%; left: Expression error: Unexpected < operator.%; height: 0; width: 0; margin: 0; padding: 0;">
Mji wa Roma
Mji wa Roma
Mahali pa mji wa Roma katika Italia
Anwani ya kijiografia: 41°54′N 12°30′E / 41.9°N 12.5°E / 41.9; 12.5
Nchi Italia
Mkoa Lazio
Idadi ya wakazi (2007)
 - 2.718.768
Tovuti: www.comune.roma.it

Roma (pia: Rumi) ndio mji mkuu wa Jamhuri ya Italia. Uko katika makutano ya mito ya Tiber na Aniene karibu na Bahari ya Mediteranea. Roma una wakazi milioni 2.7 katika eneo la 1285 km².

Ndani ya mji wa Roma lipo eneo la mji wa Vatikano ambao ni nchi ya kujitawala chini ya Papa wa Kanisa Katoliki.

Historia ya mji inasemekana imeanza rasmi tarehe 21 Aprili 753 KK, lakini majengo ya kwanza ni ya karne ya 10 K.K. Katika karne za KK ulikuwa mji mkuu wa ufalme wa Roma, halafu wa Jamhuri ya Roma, hatimaye wa Dola la Roma. Kuanzia karne ya 7 B.K. ukawa mji mkuu wa Dola la Papa, halafu wa Ufalme wa Italia na sasa wa Jamhuri ya Italia. Huitwa mara nyingi "Mji wa Milele".

Eneo la Roma[hariri | hariri chanzo]

Roma uko katikati ya Italia ikiwa mita 20 juu ya UB ndani ya tambarare ya bonde la mto Tiber linalopakana na milima ya Abruzzi, milima ya Sabino na milima ya Albani. Wilaya za jirani ni Viterbo, Rieti, L'Aquila, Frosinone na Latina. Mwanzo wa Roma ulikuwa kwenye vilima saba vilivyo katikati ya mji wa leo vinavyoitwa: Palatino, Aventino, Kapitolo, Quirinale, Viminale, Esquilini na Caeliano.

Hali ya hewa[hariri | hariri chanzo]

Hali ya hewa hutawaliwa na bahari iliyo karibu. Wastani ya halijoto kwa mwaka ni sentigredi 15,4. Mvua hunyesha wastani ya mm 758 kila mwaka.

Miezi yenye joto ni Juni hadi Agosti ikiwa na wastani ya sentigredi 21 hadi 23,8 ni miezi ya mvua kidogo.

Mwezi baridi ni Januari ikiwa na wastani wa sentigredi 7,9.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Roma ndiyo kitovu muhimu wa sekta ya viwanda na sekta ya huduma ya Italia. Utalii ni pia muhimu sana kiuchumi, kutokana na 26,100,000 watalii wanaoutembelea kwa mwaka: 6.5% za Jumla ya Pato la Taifa zinapatikana ndani ya Roma ambazo ni kushinda miji yote mingine ya Italia.

Roma ina makao makuu ya F.A.O. (Food and Agriculture Organisation - Shirika la Chakula na Kilimo) ya Umoja wa Mataifa pamoja na ofisi zote za serikali ya Italia.

Wakazi[hariri | hariri chanzo]

Roma ilianza kama muungano wa vijiji vidogo vyenye wakazi mamia kadhaa. Katika karne ya kwanza BK ilikuwa tayari na wakazi milioni moja. Tangu kuondoka kwa makao makuu ya Kaisari na kupungua kwa nguvu ya Dola la Roma katika magharibi idadi ya wakazi ilipungua hadi kuwa na takriban 100,000 mnamo mwaka 530 BK. Katika karne zilizofuata Italia pamoja na Ulaya iliona vita na mashambulio ya makabila ya washenzi. Mnamo mwaka 1000 BK Roma ilikuwa mji mdogo wa wakazi 20,000 pekee walioishi ndani ya maghofu ya mji mkubwa wa kale. Tangu kuimarika kwa utawala wa mapapa mji ulianza kukua tena mnamo mwaka 1900 Roma ikawa na wakazi 400,000. Katika karne ya 20 BK mji ulipanuka sana hadi kufika idadi ya wakazi wa zamani hata kuipita. Asilimia 7.4 ni wageni.

Orodha inayofuata inaonyesha makadirio hadi 1858, baadaye ni namba za sensa.

Mwaka BK Wakazi
330 1.000.000
410 400.000
530 100.000
650 20.000
1000 20.000
1750 156.000
1800 163.000
1820 139.900
1850 175.000
1853 175.800
1858 182.600
31. 12. 1861 194.500
31. 12. 1871 212.432
Mwaka BK Wakazi
31. 12. 1881 273.952
10. 02. 1901 422.411
10. 06. 1911 518.917
01. 12. 1921 660.235
21. 04. 1931 930.926
21. 04. 1936 1.150.589
4. 11. 1951 1.651.754
15. 10. 1961 2.188.160
24. 10. 1971 2.781.993
25. 10. 1981 2.840.259
20. 10. 1991 2.775.250
21. 10. 2001 2.546.804
31. 12. 2007 2.718.768

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Italy looking like the flag.svg Makala hii kuhusu maeneo ya Italia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Roma kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.