Uturuki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Türkiye Cumhuriyeti
Jamhuri ya Uturuki
Bendera ya Turkey Nembo ya Turkey
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Kituruki: Yurtta Sulh, Cihanda Sulh
("Amani nyumbani, amani duniani")
Wimbo wa taifa: İstiklâl Marşı
Lokeshen ya Turkey
Mji mkuu Ankara
41°1′ N 28°57′ E
Mji mkubwa nchini Istanbul
Lugha rasmi Kituruki
Serikali Jamhuri
Recep Tayyip Erdoğan
Ahmet Davutoğlu
Kuundwa kwa nchi ya kisasa
Kuundwa kwa bunge
Mwanzo wa vita ya uhuru
Ushindi
Kutangaza Jamhuri

23 Aprili 1920
19 Mei 1919
30 Agosti 1922
29 Oktoba 1923
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
780,580 km² (ya 36)
1.3
Idadi ya watu
 - 2007 kadirio
 - 2000 sensa
 - Msongamano wa watu
 
{{{population_estimate}}} (ya 17 1)
67,844,903
90/km² (ya 82 1)
Fedha Lira Mpya2 (TRY)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
EET (UTC+2)
CEST (UTC+3)
Intaneti TLD .tr
Kodi ya simu +90

-



Uturuki (Jamhuri ya Uturuki; kwa Kituruki: Türkiye Cumhuriyeti) ni nchi ya kimabara kati ya Asia na Ulaya.

Sehemu kubwa iko Asia ya magharibi lakini sehemu ndogo ya eneo lake upande wa magharibi wa Bosporus iko Ulaya.

Eneo[hariri | hariri chanzo]

Ramani ya Uturuki

Sehemu kubwa ya mipaka yake ni bahari: Mediteranea upande wa magharibi na kusini na Bahari Nyeusi upande wa kaskazini. Kwenye nchi kavu imepakana na Ugiriki na Bulgaria upande wa magharibi, Kaskazini-mashariki na Georgia, Armenia na Azerbaijan, kwa upande wa mashariki na Iran na upande wa kusini na Iraq na Syria.

Sehemu kubwa ya eneo lake ni Anatolia inayoonekana kama rasi kubwa kati ya Mediteranea na Bahari Nyeusi. Hali ya nchi ndani ya Anatolia mara nyingi ni yabisi na kilimo kinategemea umwagiliaji.

Safu za milima zinafuatana na pwani za kusini na kaskazini.

Sehemu ya mashariki ya nchi kuelekea Uajemi na Kaukazi ina milima mingi.

Maeneo ya pwani yanapokea mvua na huwa na rutuba.

Wakazi[hariri | hariri chanzo]

Uturuki una wakazi zaidi ya milioni 76. Wengi wao (70-75%) ni Waturuki.

Katika mashariki ya Uturuki watu wengi ni Wakurdi ambao ni milioni 14 au takriban 18% za raia wote wa Uturuki.

Kuna mabaki madogo tu ya Wagiriki na Waarmenia waliowahi kukalia sehemu kubwa za nchi hadi mwisho wa milki ya Osmani.

Kwenye maeneo jirani na Syria wako pia Waarabu.

Upande wa dini, karibu wote ni Waislamu, hasa kuanzia karne ya 20 ambapo Wakristo wengi waliuawa (hasa Waarmenia) au kuhama (hasa Wagiriki).

Kutokea kwa Uturuki wa kisasa[hariri | hariri chanzo]

Uturuki wa kisasa umetokea kama nchi ya pekee baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia. Waturuki waliwahi kuwa kiini cha Milki ya Osmani iliyounganisha mataifa mengi chini ya Sultani wa Konstantinopoli.

Jamhuri ya Uturuki ilianzishwa mwaka 1923 na jenerali Kemal Atatürk baada ya vita mbili. Vita ya kwanza ilikuwa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia iliyovunja Milki ya Osmani, na vita ya pili ilifuata wa kuondoa wanajeshi wa Ugiriki na nchi nyingine waliowahi kuingia ndani ya sehemu iliyokuwa imebaki baada ya kuvunjika kwa dola kubwa.

Atatürk alileta mabadiliko mengi yaliyolenga kuondoa utamaduni wa kale wa Waosmani na enzi za utawala wa sultani wa Kiislamu.

Magharibi ya nchi imeendelea sana lakini maeneo ya mashariki yamebaki nyuma.

Nchi ya kisasa[hariri | hariri chanzo]

Siku hizi Uturuki unalenga kuingia katika Umoja wa Ulaya.

Serikali ina utaratibu wa kidemokrasia ya vyama vingi. Utawala wa nchi ni kwa mikoa 81.

Mji mkuu ni Ankara ulioko katika kitovu cha Anatolia.

Mji mkubwa ni Istanbul ulioitwa zamani Konstantinopoli na zamani zaidi Bizanti: ulikuwa mji mkuu wa Dola la Uturuki hadi mwaka 1923.

Picha za Uturuki[hariri | hariri chanzo]

Turkey stub.png Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Uturuki kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Japan | Kambodia | Kazakhstan | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Kirgizstan | Laos | Lebanon | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Urusi1 | Saudia | Singapore | Sri Lanka | Syria | Taiwan (Jamhuri ya China) | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Ufilipino | Uthai | Uturuki1 | Turkmenistan | Uhindi | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi hii iko Asia lakini kwa sababu za kihistoria au kiutamaduni inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya. 3. Eneo la pekee la China.