Gibraltar

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
LocationGibraltar.png
Mwamba wa Gibraltar 2006
Ramani ya Gibraltar

Gibraltar ni eneo la ng'ambo la Uingereza ambayo ni rasi katika Mediteranea kwenye ncha ya kusini ya rasi ya Iberia katika Ulaya ya Kusini. Imapakana na Hispania.

Umuhimu wa Gibraltar[hariri | hariri chanzo]

Gibraltar imekuwa mahali muhimu tangu karne nyingi kwa sababu rasi hii iko kwenye Mlango wa Gibraltar ambako kuna km 14 za maji tu kati ya Afrika na Ulaya. Mwenye kutawala Gibraltar aliweza kutawala mwendo wa jahazi na meli kati ya Atlantiki na Mediteranea wakati wa vita. Hii ni sababu ya kwamba Uingereza ilitwaa rasi hii na kuitetea tangu mwaka 1704.

Jina la Gibraltar[hariri | hariri chanzo]

Jina la Gibraltar limetokana na uvamizi wa Waarabu wakati wa upanuzi wa Uislamu. Mwaka 711 jemadari Tariq ibn-Ziyad aliongoza jeshi lake kushambulia Hispania. Rasi inayoitwa leo "Gibraltar" ilipewa jina la "jabal at-Tariq" (mlima wa Tariq) lililokuwa baadaye "Gibraltar". Kabla ya kuja kwa Waarabu mataifa ya kale yaliita mlango huu "Nguzo za Herakles" wakitaja milima midogo ya Gibraltar na Ceuta kwa jina hili.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Gibraltar ilikuwa sehemu ya Hispania kati ya 1501 na 1704. Mwaka 1704 wakati wa vita kati ya Hispania na Uingereza ilitwaliwa na Waingereza na Waholanzi. Mwaka 1713 Hispania ilikubali kwa nafasi ya amani ya Utrecht kuwa rasi itakuwa chini ya mamlaka ya Uingereza.

Hispania imedai mara nyingi kurudishwa kwa eneo ikishtaki Uingereza kuwa na koloni ya mwisho katika Ulaya. Lakini wakazi wenyewe walipigia kura mwaka 2002 hoja la kubaki upande wa Uingereza badala ya Hispania na zaidi ya 98% wakakubali.

Mengine[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wa Gibraltar ni takriban 28,000 walio wengi huwasiliana kwa lahaja ya Kihispania lakini wote wajua Kiingereza.

Mwamba wa Gibraltar mwenye kimo cha 426 m ni mahali pa pekee Ulaya penye nyani huru.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Europa Mapa.png Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Gibraltar kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.