Katiba ya nchi inatambuliwa kuwa ni sheria kuu au ya msingi inayoweka mihimili mikuu mitatu ambayo ni Dola, Bunge na Mahakama. Inafafanua majukumu ya kila mhimili na kutoa mgawanyo wa madaraka miongoni mwa mihimili hiyo. Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniainakidhi tafsiri hiyo na ina jumla ya sura kumi.
Sura ya Kwanza inaeleza misingi mikuu ya Sera ya Taifa; Haki za Msingi na Wajibu wa Watanzania. Sura ya pili hadi ya sita inatoa masharti ya uanzishaji wa Serikali ambayo inajumuisha Dola, Bunge na Mahakama na kufafanua mgawanyo wa madaraka na kazi miongoni mwao.
Sura ya Saba inaeleza masharti kuhusu fedha za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sura ya Nane inaunda Mamlaka ya Serikali za mitaa, majiji, manispaa na wilayaza vijijini. Sura ya Tisa inatoa masharti ya kuwepo na udhibiti wa majeshi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sura ya mwisho ambayo ni Sura ya Kumi inatoa masharti mengineyo yanayohusu utaratibu wa kujiuzulu watu wanaoshika nyadhifa zilizotajwa ndani ya Katiba, pia inatoa ufafanuzi wa baadhi ya masharti yanayotumika ndani ya Katiba . Haya ndio yaliyomo ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977.
Utayarishaji na Urekebishaji wa Katiba.
Utungaji wa Katiba mpya ya nchi au dola ni mchakato tofauti na wa pekee na ule wa urekebishaji wa Katiba iliyopo. Mwenendo uliopo nchini Tanzania na nchi nyingine za Jumuiya ya Madola barani Afrika ni kwamba katiba mpya inatungwa na Bunge linalojulikana kama Bunge la Katiba; wakati urekebishaji wa katiba iliyopo unafanywa na Bunge lenyewe linalotumia taratibu maalum katika kutekeleza kazi maalumu za Bunge. Kwa maelezo zaidi tembeleaTume ya Mabadiliko ya Katiba